Thursday, September 24, 2009

Mtanzania Bingwa wa kukata viuno ndani ya Big Brother

Mshiriki mtanzania katika shindano la Big Brother, Elizabeth Gupta amekuwa kivutio kwa mwenzake kutokana na uwezo mkubwa wa kukata mauno.
Washiriki wenzake wamekuwa wakimsifia kutokana na uwezo ambao amekuwa akiuonyesha kwa kukata mauno kila unapopigwa muziki hasa ule ulio katika miondoko ya kuchezeka.

"mimi napenda sana kucheza, nataka nijiendeleze katika sanaa hadi katika ngazi ya chuo kikuu." Alisema Alizabeth wakati akiwaeleza wenzake.

Washiriki hao wamekuwa wakikaa pamoja na kucheza kwa zamu kila mmoja akionyesha uwezo alionao katika fani hiyo, na Elizabeth amekuwa kati ya kivutio kikubwa kwa wenzake.

No comments:

Post a Comment